Chama cha Ukuzaji Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) chaukidu@gmail.com

Mada Nairobi 2016

Mada/Majopo ya Kongamano la Nairobi

  1. Ukuaji na ukuzaji wa Kiswahili kuwa taaluma ya kiakademia yenye kina na mbinu zake za utafiti (kama taaluma nyinginezo za kisayansi, sayansi-jamii na sanaa-jamii)
  2. Ufundishaji wa Kiswahili kama lugha ya kigeni
  3. Ufundishaji wa Kiswahili nyumbani (elimu ya msingi, sekondari, na katika vyuo)
  4. Kiswahili na/katika vyombo vya habari
  5. Kiswahili na mitandao ya kijamii (blogu, Facebook, twitter, WhatsApp, n.k.)
  6. Fasihi ya Kiswahili (riwaya, tamthlia, ushairi)
  7. Kiswahili na muziki (wa dansi, Taarabu, kizazi kipya, n.k.)
  8. Kiswahili na sanaa za maigizo (michezo ya redioni, runingani, filamu, n.k.)
  9. Vibonzo vya Kiswahili
  10. Kiswahili na ukuaji au udororaji wa demokrasia
  11. Nafasi ya Kiswahili katika kukuza uchumi wa Afrika Mashariki
  12. Nafasi ya Kiswahili katika kuimarisha au kudhoofisha jumuiya ya Afrika ya Mashariki
  13. Nafasi ya Kiswahili katika kupanua ajira kwa vijana
  14. Utafiti na machapisho ya Kiswahili katika tanzu zake mbalimbali – isimu, lugha, fasihi, n.k.
  15. Mchango wa Kiswahili katika kukuza au kuua lugha za jamii ndogondogo
  16. Mchango wa Kiswahili katika kukuza au kuathiri Kiingereza
  17. Kiswahili na huduma za kijamii
  18. Leksikolojia na leksikografia ya Kiswahili
  19. Ufasiri na ukalimani
  20. Katiba na sheria
  21. Kiswahili mitaani (matumizi halisi) na chuoni (utafiti, ufundishaji, n.k.)
  22. Mwanafunzi wa Kiswahili: ufundishaji wa darasani ughaibuni na programu za uzamivu nyumbani
  23. Usanifishaji na uhurishaji
  24. Lahaja zinazoibukia: KiSheng, KiSwanglish, n.k.
  25. Hali ya Kiswahili nchini Rwanda, Burundi, DRC na Uganda
  26. Kusambaa kwa Kiswahili nje ya bara la Afrika
  27. Ushirikiano wa wataalamu wa Afrika Mashariki na wa ughaibuni katika utayarishaji wa matini za kufundishia Kiswahili kama lugha ya kigeni
  28. Nafasi ya teknolojia katika ufundishaji wa Kiswahili
  29. Mbinu na mikakati mipya/ibuka za kufundisha na kujifunza Kiswahili
  30. Utamaduni wa Waswahili/Kiswahili
  31. Tathmini na utahini wa Kiswahili katika madarasa ya Kiswahili kama lugha ya kigeni na kama lugha ya pili (nyumbani)
  32. Mitihani ya kutathmini uwezo wa wanafunzi wa lugha ya Kiswahili kama lugha ya kigeni