CHAUKIDU secretariat@chaukidu.org

Mnasaba wa Kiswahili na Nyuga Nyingine

MS-TCDC, Arusha, Tanzania

Kutana na wataalamu, wakereketwa, na wadau wa Kiswahili toka sehemu mbalimbali Duniani. Utafurahi kutangamana na Waswahili wengine na kuwa sehemu ya familia kubwa ya wasemaji wa Kiswahili Duniani! Mada kuu ni "Mnasaba wa Kiswahili na Nyuga Nyingine: Dira ya Mustakabali." Jioni ya tarehe 16 Disemba kutakuwa na tamasha kubwa la Utamaduni wa Mswahili ambapo watu wote wanakaribishwa, hata wale ambao hawakushiriki katika kongamano.

Twen'zetu Arusha 14 Disemba, 2023

Mada kuu ni “Mnasaba wa Kiswahili na Nyuga Nyingine: Dira ya Mustakabali.” Jioni ya tarehe 16 Disemba, kutakuwa na tamasha kubwa la Utamaduni wa Mswahili, ambapo watu wote wanakaribishwa, hata wale ambao hawakushiriki katika kongamano.

Jumuika

Kongamano la Kimataifa la CHAUKIDU linakuwa fursa ya kujumuika katika harakati za kukuza na kueneza lugha ya Kiswahili​

Wasemaji Mahiri

Kongamano hili litakupa fursa ya kusikiliza mawasilisho ya mada elekezi kutoka kwa wasemaji mahiri na waliobobea katika fani zao.

Pata Marafiki Wapya

Kongamano hili linakupa fursa ya kukutana na watu mbalimbali toka sehemu mbalimbali za dunia. Kutana na watu wapya kongamanoni!​

Hoteli na Malazi

Ili kulifurahia kongamano, utahitaji mahali pazuri pa malazi. Kamati-andalizi imewaandalia malazi ndani ya chuo cha MS TCDC na nje karibu na chuo. Japo chaguo ni lako, hakikisha unahifadhi malazi mapema ili upate mahala ambapo utapafurahia zaidi.

Wasemaji Wakuu

Prof. F.E.M.K. Senkoro

Profesa Mstaafu wa Isimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Tanzania

Prof. Jina Jina

Profesa wa Isimu ya Afrika Chuo Kikuu cha Masomo ya Kigeni cha Hankuk Korea Kusini

Maswali Yaulizwayo Sana

Katika makongamano yote ya CHAUKIDU, ikisiri hutumwa kwa mfumo maalumu wa ikisiri. Mfumo huu huwezesha upokeaji na utathmini wa ikisiri zote. Bofya hapa kutuma ikisiri yako.

Unakuwa mwanachama hai wa CHAUKIDU kwa kulipa ada ya kila mwaka. Lipa ada yako uwe mwanachama hai sasa.

Hapana. CHAUKIDU si chama cha walimu pekee. Ni chama cha wadau na wakereketwa wote wa Kiswahili.

Lipa Ada ya Kongamano

Usikose!

© Tutorim 2024. All rights reserved