Chama cha Ukuzaji Kiswahili Duniani (CHAUKIDU) chaukidu@gmail.com

Mpenzi Mwanachama Tarajali,

Mwaliko wakujiunga

Tunayo furaha kukuletea mwaliko huu wa kujiunga na CHAUKIDU, chama kitakachokuunganisha na wadau mbalimbali wa Ksiwahili duniani. Kama mmoja wa watu wenye (au watarajiao kuwa na) mahusiano na Afrika ya Mashariki, lugha ya Kiswahili na utamaduni wake, tunaamini jumuiya hii itakunufaisha. Vilevile tunaamini kuwa utaifaidisha pia jumuiya hii kwa mawazo yako na uanachama wako. Kwa hiyo, uanachama wako utakuwa ni hatua muhimu sana ya kutuwezesha kufikia moja ya malengo yetu - kuwapa watu wote duniani fursa ya kujiunga na jumuiya yenye umuhimu mkubwa.

Kama una swali lolote, tafadhali usisite kuwasiliana na Mkurugenzi Mtendaji kupitia mussahans30@gmail.com au Rais wa CHAUKIDU kupitia lubua@pitt.edu

Chagua Aina ya Uanachama

Kawaida

Uanachama unaisha Disemba 31
$ $30
00
Kwa Mwaka
  • Nje ya Afrika

Kawaida

Uanachama unaisha Disemba 31
$ $20
00
Kwa Mwaka
  • Barani Afrika

Mwanafunzi

Uanachama unaisha Disemba 31
$ $15
00
Kwa Mwaka
  • Nje ya Afrika

Mwanafunzi

Uanachama unaisha Disemba 31
$ $5
00
Kwa Mwaka
  • Barani Afrika

Asasi/Taasisi

Uanachama unaisha Disemba 31
$ $100
00
Kwa Mwaka
  • Taasisi/Asasi
Kulipia Ada ya Uanachama kwa Simu

Lipa kwa Njia Nyengine

Tunatambua uwepo wa wale ambao hawataweza kulipia ada zao kwa njia ya kadi ya benki ama PayPal. Tumeandaa utaratibu mzuri kwa watu wa nchi mbalimbali za Afrika Mashariki na wengine walioko nje ya Afrika Mashariki. Tuna wawakilishi maeneo mbalimbali na tumewapa ruhusa ya kukusanya ada kwa njia zifaazo katika nchi husika. Ulipapo ada yako kwa mwakilishi wa CHAUKIDU, ataifikisha kwa Mhazini na utapewa stakabadhi rasmi kwa malipo yako na kuingizwa katika daftari la wanachama wa CHAUKIDU. Ikiwa umelipa ada yako lakini hata baada ya wiki moja hujapata stakabadhi yako, tafadhali wasiliana na yule aliyepokea ada hiyo au uongozi wa CHAUKIDU. Majina ya wawakilishi wetu ni haya yafuatayo:

NCHIMWAKILISHI
TanzaniaDkt. Mussa Hans
KenyaProf. Iribe Mwangi
UgandaDkt. Levi Masereka
BurundiMwl. Gordien Ndayikengurukiye